• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mtwara Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mtwara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Mipango na Uratibu
      • Rasilimali watu
      • Elimu
      • Miundo Mbinu
      • Maji
    • Kitengo
      • Huduma za Kisheria
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Fedha na `Uhasibu
  • Wilaya
    • Mtwara
    • Newala
    • Tandahimba
    • Masasi
    • Nanyumbu
  • Halmashauri
    • MtwaraMC
    • MtwaraDC
    • Tandahimba
    • NewalaDC
    • MasasiDC
    • MasasiTC
    • NanyumbuDC
    • Newalatc
    • NanyambaTC
  • Uwekezaji
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Profile za Watumishi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Tukio
  • Ijuwe Mtwara

RC SAWALA AMUAPISHA DC MASASI; AMPA MAELEKEZO

Posted on: March 30th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Kanali Patrick Kenan Sawala leo tarehe 30 Machi 2025 amemuapisha Rachel Stephen Kasanda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi ambae amechukua nafasi ya Bw. Lauteri John Kanoni ambae uteuzi wake ulitenguliwa mapema wiki hii.

Kanali Sawala amempongeza Mhe. Kasanda kwa kuaminiwa tena na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuwatumikia wananchi kwa nafasi ya Ukuu wa wilaya.

“Leo umeapa na umekabidhiwa Katiba, uilinde na kuitetea; pia umekabidhiwa Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwani ni chama kinachosimamia Serikali kutekeleza majukumu.” Alieleza Kanali Sawala

Aidha Kanali Sawala amemtaka Mkuu huyo wa wilaya kufanya mikutano ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi, kutembelea miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na kutuma taarifa za utekelezaji kila mwezi.

Mhe. Kasanda pia ametakiwa kusimamia suala la elimu na kuhakikisha watoto walioandikishwa wanaripoti shule, kutokomeza utoro na kuhakikisha hali ya upatikanaji wa chakula kwa wanafunzi. Huku akitakiwa kusimamia utekelezaji wa afua za lishe ili kuondokana na utapiamlo.

Akiwa kama Mwenyekiti wa Usalama wilaya, Mhe. Kasanda ametakiwa kusimamia usalama wa raia na mali zao ikiwa ni pamoja na kudhibiti biashara za magendo hususan maeneo ya mipakani.

Mwakilishi wa Kamishna wa maadili, Bi. Esther Lemther Laizer amemtaka Mkuu huyo wa wilaya kuzingatia Haki.

Mhe. Rachel Kasanda amewahi kuwa Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa mwaka 2014 na baadae kuwa Mkuu wa Wilaya ya Katavi na Magu kwa nyakati tofauti.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MWENGE WA UHURU 2025 KUPOKELEWA MKOANI MTWARA MEI 17

    May 15, 2025
  • MTWARA TUKO TAYARI KUUPOKEA NA KUUKIMBIZA MWENGE WA UHURU 2025

    May 14, 2025
  • UFUTA NA MBAAZI KUPIMWA KIDIGITALI MKULIMA KUPATA RISTI KUPITIA SIMU YAKE

    May 14, 2025
  • MKUU WA MKOA MHE. KANALI PATRICK SAWA AKAGUA MRADI WA MAENDELEO TANDAHIMBA

    May 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

"MIRADI YA GESI KUNUFAISHA WAKAZI" MHE. DKT. DOTO BITEKO
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • IKULU
  • UTUMISHI
  • e-GA
  • MAOMBI YA KUCHOMA CHANJO YA UVIKO-19
  • SALARY SLIP
  • NBS
  • TAMISEMI

Kurasa Mashuhuri

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • WIZARA YA HABARI
  • TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Eneo kwa Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara

    Anuani ya Posta: 544, MTWARA

    Simu: +255 23 2333014

    Mobile: +255 23 2333014

    Barua Pepe: ras@mtwara.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mtwara. Haki zote zimehifadhiwa.